logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Watu 20 wafariki, 10 waokolewa baada ya basi kuzama mtoni Kitui

Basi hilo lilikuwa limebeba abiria waliokuwa wanaenda harusi.

image
na Radio Jambo

Habari04 December 2021 - 13:29

Muhtasari


•Inahofiwa huenda idadi ya waliofariki ikaongezeka uokoaji unapoendelea kwani idadi halisi ya abiria waliokuwemo bado haijathibitishwa.

Basi lililozama

Watu 18 wamethibitishwa kufariki huku wengine 10 wakiokolewa baada ya basi kuzama katika mto wa Enziu ulio eneo la Mwingi kaunti ya Kitui.

Kamanda wa polisi katika eneo hilo Joseph Yakan amesema basi hilo  la shule ya Sekondari ya Mwingi Seminary lilikuwa limebeba abiria waliokuwa wanaenda kuhudhuria harusi.

Tukio hilo linaripotiwa kutokea mwendo wa saa tano asubuhi ya Jumamosi katika kijiji cha Ngue, wadi ya Nuu.

Basi hilo lilikuwa limebeba zaidi ya  abiria 30 ambao wanasemekana kuwa wanakwaya kutoka kanisa la katoliki la Mwingi.

Katika video iliyoonekana na Radio Jambo, basi hilo lilikuwa linajaribu kuvuka daraja lililokuwa limefurika  maji wakati mikondo ya maji yenye nguvu ililibeba na kulizamisha ndani ya mto.

Kilio na nduru kubwa  kutoka kwa wanakijiji ambao walishuhudia zilitanda hewani katika eneo la tukio punde baada ya ajali hiyo ya kusikitisha kutokea. Magari mengine yalionekana kuhofia kuvuka daraja lile.

Yakan amesema kwa sasa basi hilo bado limezama kwenye matope huku akiongeza kuwa juhudi za uokoaji zinaendelea.

Inahofiwa huenda idadi ya waliofariki ikaongezeka uokoaji unapoendelea kwani idadi halisi ya abiria waliokuwemo bado haijathibitishwa.

Mengi yanafuata...


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved