logo

NOW ON AIR

Listen in Live

SRC yaondoa marupu rupu ya wabunge kuhudhuria vikao vya bunge

Mbali na mshahara wabunge na nchini Kenya hulipwa marupurupu ya shilingi 5000 kila kikao cha bunge wanachohudhuria.

image
na Radio Jambo

Habari28 July 2022 - 11:38

Muhtasari


• Tume ya kudhibiti mishahara nchini Kenya, SRC imetangaza kuondoa marupurupu yanayolipwa wabunge kila wanapohudhuria vikao vya bunge.

Mwenyekiti wa SRC Lyn Mengich Picha: MAKTABA

Tume ya kudhibiti mishahara nchini Kenya, SRC imetangaza kuondoa marupurupu yanayolipwa wabunge kila wanapohudhuria vikao vya bunge.

Mwenyekiti Lyn Mengich alitangaza hatua hiyo wakati wa mkutano na Chama cha Wahariri mjini Nairobi siku ya Alhamisi.

Mbali na mshahara wabunge na maseneta nchini Kenya hulipwa marupurupu ya shilingi 5000 kwa kila kikao cha bunge wanachohudhuria. 

Mengich alisema kwamba marufuku hiyo inaanza kutekelezwa kuanzia Agosti 9. 

Kulingana na SRC marufuku hii pia itaathiri Maspika na mawaziri katika serikali za kaunti. 

Mengich alibainisha kuwa marupurupu yaliyositishwa ni pamoja na yale ya usafiri kwa maeneo bunge na ruzuku ya magari kwa Maafisa wote wa Serikali.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved