logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Nilikuwa nasubiri Raila na Wanjigi nilipokamatwa-Miguna

Miguna alifurushwa nchin tangu wakati huo, na kurejea nchini 20 Oktoba 2022.

image
na Radio Jambo

Makala04 November 2022 - 16:30

Muhtasari


  • Alisema ni watatu tu ndio wanajua walichopanga kufanya siku hiyo. Watatu hao walikuwa wamepanga kukutana saa nane kamili
Jenerali Miguna hatimaye ametua nchini

Wakili Miguna Miguna amefichua kwamba alipokamatwa 2018, alikuwa nyumbani kwake Runda akiwasubiri Raila Odinga na mshirika wake wakati huo Jimi Wanjigi.

Alisema ni watatu tu ndio wanajua walichopanga kufanya siku hiyo. Watatu hao walikuwa wamepanga kukutana saa nane kamili.

"Siku nilipokamatwa kutoka nyumbani kwangu, nilikuwa nikisubiri Raila aje lakini badala yake polisi walikuja. Nilikuwa nikimsubiri yeye na Wanjigi, wanajua tulichokuwa tumepanga kufanya," Miguna alisema.

Wakili huyo alizungumza Ijumaa alipokuwa akiwahutubia wakazi wa Magina, eneo la Nyando, Kaunti ya Kisumu.

Kukamatwa kwa Miguna mnamo 2018 kufuatia kuapishwa  kwa Raila Odinga katika bustani ya Uhuru jijini Nairobi, ambapo aliapisha.

Miguna alifurushwa nchin tangu wakati huo, na kurejea nchini 20 Oktoba 2022.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved