logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Linturi ajitenga na matamshi ya Kuria kuhusu uingizaji wa mahindi kutoka nje ya nchi

Linturi alisema kwammba atatoa ripoti ya kina kuhusu chakula, atakapokuwa na data kamili.

image
na

Habari28 November 2022 - 11:42

Muhtasari


  • “Kwa hiyo sitajibu kinachoripotiwa kwenye mitandao ya kijamii,” alisema.
  • "Shika farasi wako maana nataka kukupa msimamo ambao niko tayari kuutetea. Nahitaji kuwa na takwimu kabla sijajibu hilo."

Waziri wa Kilimo Mithika Linturi amejitenga na maoni ya Waziri wa Biashara Moses Kuria kuhusu uingizaji wa mahindi.

Linturi amesema yeye ndiye mlinzi wa kiasi gani cha chakula tunachohitaji na upungufu ni kiasi gani.

“Kwa hiyo sitajibu kinachoripotiwa kwenye mitandao ya kijamii,” alisema.

"Shika farasi wako maana nataka kukupa msimamo ambao niko tayari kuutetea. Nahitaji kuwa na takwimu kabla sijajibu hilo."

Linturi alisema kwammba atatoa ripoti ya kina kuhusu chakula, atakapokuwa na data kamili.

"Nitatoa ripoti ya kina zaidi kuhusu hali ya chakula kitaifa baadaye nikiwa na data yote. Tulia, utakuwa na chakula," Linturi alisema.

Waziri Kuria amekuwa akikosolewa  vikali mitandaoni baada ya matamshi yake ya uingizaji mahindi.

Jumamosi Kuria aliwapa wakulima saa 72 ili kutoa mahindi yaliyokuwa yamehifadhiwa la si vyo mahindi kutoka nje ya nchi yaingizwe.

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved