In Summary
  • Akizungumza wakati wa uzinduzi wa Mto Nairobi, Ruto alisema serikali imejaribu iwezavyo kupunguza gharama ya maisha nchini
Andrew Kibe apinga maombi ya rais Ruto Nyayo.
Image: Facebook, Maktaba

Rais William Ruto amesema utawala wake utashusha bei ya Unga hadi Sh120 lakini wanahitaji muda kufanya hivyo.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa Mto Nairobi, Ruto alisema serikali imejaribu iwezavyo kupunguza gharama ya maisha nchini.

"Bei ya unga ilikua Sh230, sai tumeteremsha hadi Sh180, kwa hivyo mtupee nafasi bei iteremke hadi Sh140, mpaka wakati itafika Sh120,"Alizungumza Ruto.

Ruto pia alisema alirithi madeni kutoka kwa utawala wa Rais Mstaafu Uhuru Kenyatta.

"Walituwacha na madeni kibao, karibu inchi yetu iteleze, saa hizi tumeanza kupunguza madeni."

Kufikia Agosti 2022, gharama ya maisha nchini Kenya ilipanda hadi kupanda kwa bei ya juu ya vyakula na mafuta kwa miaka mitano pamoja na gharama ya vifaa vya nyumbani.

Ofisi ya Kitaifa ya Takwimu ya Kenya (KNBS) ilionyesha kiwango cha gharama ya maisha katika miezi 12 iliyopita ilipanda kwa pointi 20 hadi asilimia 8.5 kutoka asilimia 8.3 mwezi Julai.

Inaadhimisha mwezi wa tatu mfululizo ambapo gharama ya maisha ya mwaka baada ya mwaka ilivuka kiwango cha juu cha lengo la asilimia 7.5, hali iliyoshuhudiwa mara ya mwisho miaka mitano wakati nchi ilipopiga kura za urais.

 

 

 

 

 

 

View Comments