logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Tanzia:Aliyekuwa mkewe waziri Ababu Namwamba aaga dunia

Kifo chake kilithibitishwa na jamaa zake wa karibu, ambao hawakutaja kiini cha kifo.

image
na Radio Jambo

Makala08 March 2023 - 09:57

Muhtasari


  • Kulingana na familia yake, Marehemu alikuwa amesherehekea siku yake ya kuzaliwa siku ya Jumanne, Machi 7, saa chache kabla ya kifo chake cha ghafla.
  • Mwili wake unasemekana kuhamishiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti cha MP Shah jijini Nairobi

Priscah Mwaro, aliyekuwa mke wa Waziri wa Michezo na Sanaa Ababu Namwamba amefariki jijini Nairobi.

Kifo chake kilithibitishwa na jamaa zake wa karibu, ambao hawakufichua maelezo zaidi.

Mwili wake unasemekana kuhamishiwa chumba cha kuhifadhi maiti cha MP Shah jijini Nairobi.

Priscah alikuwa mke wa Ababu kwa miaka mitatu, na kubarikiwa watoto watatu. Wawili hao walikosana na kutengana.

Kulingana na familia yake, marehemu alikuwa amesherehekea siku yake ya kuzaliwa siku ya Jumanne, Machi 7, saa chache kabla ya kifo chake cha ghafla.

Aidha, familia ilisema kwamba Mwaro amepitia mengi katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita.

Kutoka kwetu hapa Radio Jambo Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved