logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Afueni kwa Matiang'i baada ya DPP kukataa mashtaka dhidi yake

DCI ilikuwa imetuma faili kwa DPP kukagua na kupendekeza kufunguliwa mashtaka

image
na Radio Jambo

Makala13 March 2023 - 08:41

Muhtasari


  • Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma aligundua kuwa ushahidi uliotolewa haukutosha kuendeleza mashtaka
Fred Matiang'i

Aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani Fred Matiang’i hatashtakiwa kortini kutokana na kuchapishwa kwa habari kuhusu madai ya kuvamiwa na polisi katika nyumba yake ya Karen mnamo Februari 8.

Hii ni baada ya Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma (ODPP) kusema kuwa ushahidi uliotolewa na Kurugenzi ya Upelelezi wa Jinai (DCI) dhidi ya Matiang’i na Wakili wake Danstan Omari hautoshi kuendeleza mashtaka hayo.

“Baada ya uchambuzi huru na wa kina wa ushahidi uliotolewa na uhakiki wa maelezo ya mashahidi, Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma aligundua kuwa ushahidi uliotolewa haukutosha kuendeleza mashtaka yaliyotajwa hapo juu dhidi ya Dkt. Fred Okeng’o Matiang’i na wakili Bw. Danstan Omari. Ushahidi uliotolewa haukukidhi viambajengo vinavyohitajika kuthibitisha kila kosa lililotajwa kama inavyotakiwa kisheria,” ODPP alisema.

Katika taarifa kwa vyombo vya habari, ODPP aliagiza DCI kufunga faili ya uchunguzi bila hatua nyingine za polisi.

DCI ilikuwa imetuma faili kwa DPP kukagua na kupendekeza kufunguliwa mashtaka kwa wawili hao kwa makosa ya; Kula njama za kutenda kosa kinyume na kifungu cha 393 cha Kanuni ya Adhabu na Uchapishaji wa taarifa za uongo kinyume na kifungu cha 23 cha Sheria ya Kompyuta na Matumizi Mabaya na Makosa ya Mtandao namba 5 ya mwaka 2018.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved