logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Watalii wawili wa kigeni wafariki katika ajali ya Maasai Mara nchini Kenya

Ajali hiyo ilitokea baada ya gari lao lilipokwama na kupoteza mwelekeo, polisi walisema.

image
na Radio Jambo

Makala14 March 2023 - 04:28

Muhtasari


• Hifadhi ya taifa ya Maasai Mara ni kivutio maarufu cha utalii kwa wenyeji na wageni.

Gari lao lilikwama na kupoteza mwelekeo (picha ya faili)

Watalii wawili wa kigeni, Mjerumani na Mswizi, walifariki katika ajali katika mbuga ya wanyama ya Maasai Mara nchini Kenya siku ya Jumamosi.

Ajali hiyo ilitokea baada ya gari walilokuwa wakitumia kwa ziara yao kukwama na kupoteza mwelekeo, polisi walisema.

Gari hilo lilikuwa limebeba raia watatu wa Ujerumani na wawili wa Uswizi, wakati ajali hiyo ilipotokea kando ya daraja la Sekenani-Mara.

Mtalii mwingine mmoja alijeruhiwa na wengine wawili walinusurika bila majeraha. Mtalii aliyejeruhiwa alisafirishwa kwa ndege hadi hospitali katika mji mkuu wa Kenya, Nairobi, vyombo vya habari vya ndani vilisema.

Polisi wa Kenya walisema ajali hiyo inachunguzwa.

Hifadhi ya taifa ya Maasai Mara ni kivutio maarufu cha utalii kwa wenyeji na wageni.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved