logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Meta yazuiwa kuwafuta kazi wasimamizi wa maudhui wa Facebook nchini Kenya

Meta na Sama wamepewa siku saba wawe wametoa jibu kuhusu ombi hilo

image
na Radio Jambo

Makala23 March 2023 - 18:08

Muhtasari


  • Mahakama ya kazi pia imeizuia Meta na kampuni yake yaajira, Sama, kuwaajiri wasimamizi wengine wa kuchukua nafasi ya wale waliofutwa kazi.

Mahakama katika mji mkuu wa Kenya Nairobi, imeizuia kampuni ya Meta, ambayo ni kampuni mama ya facebook, kuwafuta kazi wasimamizi wake wa maudhui huku wakisubiri kusikilizwa kwa kesi ya kupinga hatua ya kufutwa kwao kazi.

Mahakama ya kazi pia imeizuia Meta na kampuni yake yaajira, Sama, kuwaajiri wasimamizi wengine wa kuchukua nafasi ya wale waliofutwa kazi.

Shitaka hilo liliwasilishwa na wasimamizi wa maudhui ya Facebook 43 nchini Kenya , waliokuwa wameajiriwa na Sama kwa niaba ya Meta. Wanadai kwamba shughuli ya kuwasimamisha kazi inayofanyika ni kinyume cha sheria.

Wazimamizi waliiambia mahakama kwamba wamepewamaelezo ‘’tofauti na ya ‘’kukanganya "ya kuwataka waache kazi, limeripoti gazeti la Daily Nation.

Takriban wasimamizi 260 wa maudhui walitarajiwa kufutwa kazi, kulingana na vyombo vya habari nchini Kenya.

Meta na Sama wamepewa siku saba wawe wametoa jibu kuhusu ombi hilo

Kesi hiyo itasikilizwa tarehe 28 Machi.

 

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved