logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Habari za hivi sasa - Mjane wa Dedan Kimathi, Mukami Kimathi afariki, 96

Alifariki alipokuwa akipokea matibabu katika hospitali baada ya kupata matatizo ya kupumua.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri05 May 2023 - 05:27

Muhtasari


• Alifariki alipokuwa akipokea matibabu katika hospitali moja jijini Nairobi baada ya kupata matatizo ya kupumua.

Mjane wa shujaa wa Mau Mau Dedan Kimathi, Mukami Kimathi.

Mjane wa shujaa wa kupigania uhuru wa taifa la Kenya, Field Marshal Dedan Kimathi, Mukami Kimathi amefariki.

Mama Mukami ambaye pia ni shujaa wa ukombozi wa Kenya kutoka minyororo ya ukoloni amefariki akiwa na umri wa miaka 96.

Alifariki alipokuwa akipokea matibabu katika hospitali moja jijini Nairobi baada ya kupata matatizo ya kupumua.

Kulingana na bintiye Everlyn Kimathi Wangui, mama Mukami alifariki usiku wa kuamkia Ijumaa .

Mukami atakumbukwa sana kwa mchango wake wakati wa harakati za kupigania uhuru wa Kenya. Alikuwa miongoni mwa wanawake shujaa waliokuwa wakiwapelekea chakula wapiganaji wa Mau Mau wakiwa msituni.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved