logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Baadhi ya wahasiriwa wa Shakahola huenda waliuawa mahali pengine - Haki Africa

"Tunashuku kuwa kuna uwezekano mkubwa kwamba hawa walikuwa wahasiriwa wa magenge au unyanyasaji wa polisi." Khalid alisema.

image
na

Makala16 May 2023 - 04:01

Muhtasari


•Khalid alisema kwa kuzingatia matokeo ya uchunguzi wa maiti, baadhi ya miili inaweza kuwa ya wahasiriwa wa ukatili wa polisi au wa magenge.

•Khalid anasema baadhi ya wauaji huenda walichukua fursa ya hali hiyo na kuwaua watu kisha kutupa miili yao msituni.

waanza kuopoa miili ya watu wanaoaminika kuwa wafuasi wa kasisi wa Malindi Paul Mackenzie katika eneo bunge la Shakahola Magarini kaunti ya Kilifi.

Huenda baadhi ya miili zaidi ya 200 iliyofukuliwa katika Msitu wa Shakahola katika Kaunti ya Kilifi haihusiani na dhehebu linalodaiwa la mchungaji Paul Mackenzie.

Haya ni kwa mujibu wa Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la haki za binadamu la Haki Africa Hussein Khalid.

Khalid alisema kwa kuzingatia matokeo ya uchunguzi wa maiti, baadhi ya miili inaweza kuwa ya wahasiriwa wa ukatili wa polisi au wa magenge.

"Wengi wa waathiriwa walikufa kutokana na njaa kulingana na ripoti ya uchunguzi wa maiti ya Mwanapatholojia wa Serikali Johansen Oduor lakini takriban 30% -40% hawakufa kwa njaa kumaanisha kuwa wangekuwa hawahusiani na imani ya kidini," aliambia Star.

"Tunashuku kuwa kuna uwezekano mkubwa kwamba hawa walikuwa wahasiriwa wa magenge au unyanyasaji wa polisi."

Ripoti ya uchunguzi wa maiti ya mwanapatholojia wa serikali inaonyesha kuwa wengi wa waathiriwa walikufa kutokana na njaa, kunyongwa huku wengine wakipigwa na kitu butu.

Idadi ya waliofariki sasa imefikia 201 huku vyombo vya usalama vikisema miili zaidi bado haijafukuliwa.

Zaidi ya watu 601 wameripotiwa kupotea; kwa hivyo idadi ya miili inatarajiwa kuongezeka.

Haki Africa pia inataka tume ya uchunguzi iliyoundwa na Rais William Ruto kuangazia vyombo vingine visivyohusishwa na mafundisho ya Mackenzie. Tume hiyo inaongozwa na Lady Jaji Jessie Lessit.

Khalid anasema baadhi ya wauaji huenda walichukua fursa ya hali hiyo na kuwaua watu kisha kutupa miili yao msituni.

"Lazima kuwe na watu binafsi, wanasiasa, polisi au wauaji ambao hawakufurahishwa na wengine na kuchukua fursa hiyo. Kutokana na uchunguzi wa maiti, tunaweza kuthibitisha kwamba kulikuwa na mauaji na sio njaa tu," Khalid alieleza.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved