logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Canada yakanusha kutoa fursa ya ajira kwa Wakenya

Huu ni uongo, na programu za uhamiaji zilizotajwa hazipo," IRCC ilisema katika taarifa.

image
na Radio Jambo

Makala17 May 2023 - 09:14

Muhtasari


  • Haya yanajiri kufuatia tangazo la Waziri wa Mambo ya Nje wa Kenya Alfred Mutua Jumanne kwamba Wakenya sasa wataweza kwenda kuishi au kufanya kazi nchini Canada.

Serikali ya Canada imekanusha ripoti kuwa Wakenya sasa wanaweza kusafiri hadi nchini humo kutafuta nafasi za kazi.

Haya yanajiri kufuatia tangazo la Waziri wa Mambo ya Nje wa Kenya Alfred Mutua Jumanne kwamba Wakenya sasa wataweza kwenda kuishi au kufanya kazi nchini Canada.

Waziri Mutua, ambaye alikuwa katika ziara rasmi nchini, alisema alifanya mkutano na Waziri wa Uhamiaji, Wakimbizi na Uraia wa Canada (IRCC) Sean Fraser na kukubaliana kuhusu fursa mbalimbali za uhamiaji.

Alisema mchakato kwa wanaotaka kwenda Canada ni rahisi lakini unahitaji bidii. "Taarifa potofu zinasambaa ambazo zinapendekeza kuwa programu maalum zinakaribisha wahamiaji wa Kenya.

Huu ni uongo, na programu za uhamiaji zilizotajwa hazipo," IRCC ilisema katika taarifa.

IRCC ilisema kwa taarifa sahihi kuhusu jinsi ya kuhamia Canada, Wakenya wanapaswa kutembelea tovuti ya uhamiaji nchini humo.

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved