logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Maseneta Sifuna na Khalwale kuongoza mazungumzo kuhusu IEBC

Wawakilishi wa Azimio ni maseneta Edwin Sifuna, Enoch Wambua na Mbunge Millie Odhiambo.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri17 May 2023 - 14:15

Muhtasari


• Ujumbe wa Kenya Kwanza utajumuisha Seneta wa Bomet Hillary Sigei, Seneta wa Kakamega Boni Khalwale na Mbunge wa Kibwezi Magharibi Mwengi Mutuse.

b6251efb2cdb00bc

Kamati ya pande mbili inayoshirikisha miungano ya Kenya kwanza na Azimio imeunda kamati ndogo ya wanachama sita kujadili mageuzi katika tume ya IEBC.

Akihutubia wanahabari, mwenyekiti mwenza wa kamati hiyo ya pande mbili Otiende Amollo alisema Seneta wa Nairobi Edwin Sifuna ataongoza upande wa Azimio, huku Seneta wa Kakamega Boni Khalwale akiongoza upande wa Kenya Kwanza.

Wawakilishi wa Azimio ni kama ifuatavyo: Seneta wa Nairobi Edwin Sifuna, Seneta wa Kitui Enoch Wambua na Mbunge wa Suba Kaskazini Millie Odhiambo.

Ujumbe wa Kenya Kwanza utajumuisha Seneta wa Bomet Hillary Sigei, Seneta wa Kakamega Boni Khalwale na Mbunge wa Kibwezi Magharibi Mwengi Mutuse.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved