logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Hatimaye rais Ruto amkumbuka aliyekuwa waziri wa michezo Rashid Echeza

Echesa alitimuliwa serikalini 2019 kutokana na madai ya ubadhirifu wa fedha katika wizara yake.

image
na Radio Jambo

Habari19 May 2023 - 08:49

Muhtasari


• Kwa mujibu wa notisi ya gazeti la serikali ya Mei 19, 2023, Echesa itahudumu kwa muda wa miaka mitatu, kuanzia tarehe 19 Mei 2023.

Aliyekuwa waziri wa Michezo Rashid Echesa

Rais William Ruto amemteua aliyekuwa Waziri wa Michezo Rashid Echesa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya kitaifa ya Chemichemi za maji  ( Kenya Water Towers Board.

Kwa mujibu wa notisi ya gazeti la serikali ya Mei 19, 2023, Echesa itahudumu kwa muda wa miaka mitatu, kuanzia tarehe 19 Mei 2023.

Echesa alihudumu kama waziri wa michezo katika serikali ya rais Mustaafu Uhuru Kenyatta, lakini alitimuliwa kutokana na madai ya utepetevu na ubadhirifu wa fedha katika wizara yake  mwaka 2019.

==========

Echesa alikabiliwa na sakata kadhaa wakati wa utawala wa rais mustaafu Uhuru Kenyatta. Disemba 2021, mahakama ya Nairobi ilimuachilia huru katika kesi ya  kashfa ya silaha feki yenye thamani ya shilingi bilioni 39.

Hakimu Mkuu Mwandamizi Kenneth Cheruiyot alimwachilia kwa misingi kwamba mkurugenzi wa mashtaka ya umma alikosa kuwasilisha mashahidi muhimu katika kesi hiyo. 

Cheruyoit aliamua kuwa hakuna ushahidi wa kuwaweka washtakiwa katika utetezi wao.

Echesa alikuwa ameshtakiwa kwa kupanga njama ya kutenda uhalifu, Kupata pesa kwa njia ya udanganyifu.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved