In Summary
  • Bei mpya za mafuta zitaanza kutumika kuanzia saa sita usiku Jumamosi, Julai 1, 2023, licha ya Sheria ya Fedha kusimamishwa.
Mhudumu akiweka gari Mafuta ya petroli
Image: MAKTABA

Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Petroli (EPRA) mnamo Ijumaa, 30, ilitangaza bei mpya za mafuta kwa Julai 2023.

Bei hizo zilipitiwa upya kufuatia kuongezeka maradufu kwa ushuru wa ongezeko la thamani (VAT) kwenye mafuta kutoka asilimia 8 hadi 16.

Jijini Nairobi, bei mpya zitauzwa kama ifuatavyo; petroli  Ksh195.53 kwa lita, dizeli Ksh179.67 na mafuta ya taa Ksh173.44 kwa lita.

Bei mpya za mafuta zitaanza kutumika kuanzia saa sita usiku Jumamosi, Julai 1, 2023, licha ya Sheria ya Fedha kusimamishwa.

"Kwa mujibu wa Sheria ya Fedha, 2023, Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) kwenye Super Petrol (PMS), Dizeli (AGO) na Mafuta ya Taa (IK) imefanyiwa marekebisho kutoka asilimia 8 hadi 16 kuanzia tarehe 1 Julai 2023.

"Kwa hiyo, Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati ya Petroli (EPRA) imefanya mahesabu ya bei ya juu zaidi ya pampu ambayo itaanza kutumika kuanzia tarehe 1 Julai hadi 14 Julai 2023 kwa kuzingatia VAT kwa asilimia 16," ilisomeka sehemu ya taarifa ya EPRA.

“Madhumuni ya Kanuni za Upangaji Bei ya Petroli ni kupunguza bei za reja reja za mafuta ya petroli ambayo tayari yapo nchini ili uagizaji wa bidhaa na gharama nyinginezo zilizotumika kwa uangalifu zirejeshwe huku ikihakikisha bei nzuri kwa watumiaji.

 

 

 

 

 

View Comments