logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mwanamke ajisalimisha kwa kumuua mpenziwe kwa kumduga kisu

Alimdunga kisu mara tano kwenye mapaja na katika sehemu za siri.

image
na Radio Jambo

Habari12 September 2023 - 07:15

Muhtasari


• Polisi kujunguza kifo cha mwanamke aliyemduga mpenzi wake na kujisalimisha

Crime scene

Mwanamke mmoja amejisalimisha kwa polisi baada ya kumuua mpenzi wake kwa kumdunga kisu katika kaunti ya Kirinyaga.

Hofu  imetanda katika  kituo cha kibiashara cha Kagio kaunti ya Kirinyaga baada ya mwanamke mwenye umri wa miaka 38 kumuua mpenziwe kwa kumdunga kisu mara tano.

Kulingana na kamanda wa polisi wa kaunti ndogo ya Kirinyaga Magharibi Moses Koskei, mwanamke huyo ambaye ni mhudumu wa baa katika kituo hicho cha biashara alijisalimisha katika kituo cha polisi cha Kagio siku ya Jumatatu baada ya kisa hicho.

“Alimdunga kisu mpenzi wake mara tano; mara mbili kwenye paja la kushoto, mara mbili kwenye paja lake la kulia na mara ya tano katika sehemu zake za siri,” Koskei alisema.

Koskei alisema mwanamume huyo alifariki baada ya kuvuja damu na polisi wanachunguza sababu ya mwanamke huyo alimuua mpenzi wake.

"Wawili hao wamekodisha nyumba kando ya Barabara ya Baricho katika kituo hiki cha kibiashara na tunaambiwa wote wanatoka eneo bunge la Gichugu," Koskei alisema.

Mkuu wa polisi alisema bado hawajapata kisu cha muuaji.

"Tunamtarajia mshukiwa ambaye anazuiliwa katika kituo cha polisi cha Kagio atuambie alificha wapi silaha ambayo tutaitumia kama ushahidi," Koskei alisema.

Mwili wa mhasiriwa ulipelekwa katika hifadhi ya maiti ya Hospitali ya Rufaa ya Kerugoya.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved