In Summary

• Njeng'ere alizungumza Alhamisi katika Jumba la Mtihani jijini Nairobi ambapo Waziri wa Elimu Ezekiel Machogu alikuwa kitoa matokeo ya KCPE 2023.

• “Baraza litawaandalia watahiniwa wa KCPE ambao walikuwa wamejiandikisha lakini hawakuweza kufanya mitihani yao, kufanya hivyo baada ya siku 30,”

Image: HISANI

Mkurugenzi Mtendaji wa KNEC David Njeng'ere amesema wanafunzi wa Darasa la Nane ambao walikuwa wamejiandikisha kwa mtihani wa KCPE wa 2023 lakini wakakosa kufanya watapata nafasi ya pili baada ya siku 30.

Njeng'ere alizungumza Alhamisi katika Jumba la Mtihani jijini Nairobi ambapo Waziri wa Elimu Ezekiel Machogu alikuwa kitoa matokeo ya KCPE 2023.

“Baraza litawaandalia watahiniwa wa KCPE ambao walikuwa wamejiandikisha lakini hawakuweza kufanya mitihani yao, kufanya hivyo baada ya siku 30,” akasema.

Machogu alisema watahiniwa hao 9,354 watafanyiwa mitihani maalum Januari.

Njeng'ere alibainisha kuwa tangu 1985, vikundi 39 vimefanya Mitihani ya KCPE, huku hakiki mbili kuu zikifanywa kuhusu majaribio yaliyotumiwa.

"Tangu kuanzishwa, Mtihani wa KCPE umetolewa kwa zaidi ya watahiniwa 26,316,037 katika kipindi cha miaka 39 iliyopita. Watahiniwa wa hali ya ukimbizi na wengine wasio raia wa Kenya wamefanya mtihani huo," alisema.

Bosi huyo wa Knec alisema kuanzia 2005 hadi 2008 KCPE pia ilitolewa kwa raia wa Sudan Kusini wa eneo la milima ya Kauda. Kwa jumla, watu  103,779 wasio raia wa Kenya wameidhinishwa baada ya kumaliza KCPE.

Vile vile, watahiniwa 25,000 wenye ulemavu wamefanya Mitihani ya KCPE kwa muda wa miaka 39 iliyofanywa.

Alisema usawa wa kijinsia wa watahiniwa wa KCPE mwaka wa 1985 ulikuwa 59.2% na 40.8% kwa watahiniwa wa kiume na wa kike mtawalia.

"Uwiano huu uliongezeka kwa miaka mingi na kuanzia 2013 hadi 2022, jinsia zote mbili zilikuwa sawa. Hata hivyo, mwaka 2023, usawa wa kijinsia umeshuka huku watahiniwa wa kike wakiwa 48.70% na wanaume 51.3%," alisema.

Zaidi ya hayo, aliwashukuru maafisa wote wa nyanjani waliotoa huduma zao kuhakikisha shughuli nzima za mitihani ya KCPE zimefaulu mwaka huu.

"Ningependa kutaja hasa, kwa shukrani za Katibu wa Baraza la Mawaziri, timu ya Elimu ya Kaunti ya Vihiga kwa kazi yao nzuri ya kusajili watahiniwa wa KCPE wa 2023 kwa njia ya kielektroniki," alisema.

Kutokana na hali hiyo, alisema kaunti hiyo haikuwa na kesi za kuchelewa kwa usajili.

Alizitaka kaunti zingine zote kuiga uongozi huu wa kupigiwa mfano.

Njeng'ere pia aliwashukuru wasimamizi 28,533 wa vituo vya KCPE ambao walihakikisha kwamba KCPE na KPSEA zinafanyika katika vituo bila , licha ya hali mbaya ya anga ambayo inaendelea kushuhudiwa katika maeneo mbali mbali nchini

Alisema KNEC ilihusisha huduma za watahini 5,692 wakati wa uwekaji alama wa Utunzi wa Kiingereza, Kiswahili Insha, na Utunzi wa Lugha ya Ishara ya Kenya.

Alisema kama kuonyesha shukrani, KNEC imetoa vyeti vya shukrani kwa watahini wote wanaohusika na kusahihisha utunzi wa Kiingereza  na Insha.

View Comments