logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Sitaki handshake! Raila amzima Ruto na washirika wa Kenya Kwanza

Raila alisema kwamba yuko tayari kukufa akipigania haki yake.

image
na Radio Jambo

Makala23 January 2023 - 12:35

Muhtasari


  • Ruto alisema hatakubali matakwa yake kwani Upinzani unafanya maandamano kuhusu ripoti ya wizi wa IEBC

Kiongozi wa Azimio-One Kenya, Raila Odinga amemjibu Rais William Ruto na washirika wake kuhusu madai ya kutaka handshake.

Akizungumza Jumatatu, Raila alikosoa matamshi hayo ambayo yalitolewa na upande wa Kenya Kwanza wikendi. 

Siku ya Jumapili, Ruto na washirika wake walidai kuwa mkutano wa Kamukunji ulikuwa mpango wa Raila kuchafua serikali ili kuafikiana naye.

Ruto alisema hatakubali matakwa yake kwani Upinzani unafanya maandamano kuhusu ripoti ya wizi wa IEBC.

“Sitaruhusu watu wachache kuwatendea Wakenya kwenye mikutano ili tuache kuwatumikia wananchi na kuwafanyia kazi. Mwisho umefika; hakuna zaidi. Ulichopata kutokana na vitisho kinafaa kutosha kwa sababu hatuwezi kufanya kazi kwa watu wachache mwaka hadi mwaka,” Rais alisema.

Raila alisema kwamba yuko tayari kukufa akipigania haki yake.

"Ruto na huyo Gachagua wake, wacheni upuzi , Kenya si yenu,Hatuwezi kutishwa na bwana Ruto na bwana Gachagua. Sisi ni wakenya na tutabaki Kenya hii. Wameiba ushindi wetu na sitaki waongeze matusi. Sisi tunadai haki yetu na tuko tayari kukufa kupigania haki yetu."Raila alisema.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved