07 June 2019 1 Min Read
Rais wa CAF aachiliwa huru Ufaransa
by Yusuf Juma Michezo
Rais wa shirikisho la soka barani afrika Ahmad Ahmad, ameachiliwa huru nchini Ufaransa bila kufunguliwa mashtaka yoyote baada ya kuhojiwa huko Marseille ,mwendesha mashtaka mjini humo amesema .
Xavier Tarabeux amesema Ahmad, aliyekuwa nchini Ufaransa kwa mkutano wa Fifa uliofanyika siku ya jumatano alihojiwa katika sehemu ya uchunguzi kuhusu ufisadi na ulagjai wa kughushi stakabadhi .