Theo Walcott ni miongoni mwa wachezaji wa Everton waliowasili nchini
Mshambulizi matata wa Everton na timu ya taifa ya Uingereza, Theo Walcott ni miongoni mwa wachezaji sugu wa Everton ambao wamewasili nchini hii leo, tayari kumenyana na Kariobangi Sharks katika mechi ya kirafiki hapo kesho.
Mchezaji huyo ambaye alijishindia nyoyo za mashabiki wengi haswa kina dada wakti alipokuwa akizitikisa nyavu katika klabu ya Arsenal, alionekana mchangamfu pindi tu ndege ya timu hiyo ilivyotua.
Kikosi hicho cha Marcos Silva kinatumia mechi hii kama mojawapo ya maandalizi kemkem kabla ya msimu mpya ujao.
Everton ilimaliza msimu uliopita ikiwa katika nafasi ya nane ndani ya ligi kuu ya Uingereza baada ya kujizolea alama 54.
The Blues watamenyana na kikosi cha Kariobangi Sharks katika uga wa Kasarani siku ya Jumapili mida ya saa nane mchana. The Toffees wanarejea Afrika Mashariki miaka miwili baada ya kutembea Tanzania ambapo walicheza na Gor Mahia.
Kikosi cha Everton ambacho kimewasili Nairobi:
Maarten Stekelenburg
Jonas Lossl
Mason Holgate
Lewis Gibson
Morgan Schneiderlin
Dennis Adeniran
Tom Davies
Theo Walcott
Ademola Lookman
Leighton Baines
Andre Gomes
Oumar Niasse
Ryan Astley
Callum Connolly
Morgan Feeney
Antonee Robinson
Beni Baningime
Joe Williams
Nathan Broadhead
Fraser Hornby
Josh Bowler
Nathangelo Markelo