- gani kali
- ALGERIA TEAM

Nigeria na Senegal tayari zimefuzu kwa nusu fainali ya mashindano ya kombe la  afcon na leo tutafahamu zitachuana na timu gani.  Makabiliano  makali yananukia leo kati ya Ivory coast  na  Algeria ,miamba wazito wa soka barani ambapo wengi wanatabiri huenda matuta ya penalty ndio yatakayoamua mshindi .

Mechi hiyo itaanza  saa moja jioni na itapeperushwa mubashara hapa radio Jambo .Baadaye mwendo wa saa nne usiku   Vijana wapya katika kipute hicho  Madagascar wanajipima maarifa dhidi ya vigogo Tunisia  huezi kujua matokeo yatakuwa yepi.

Tayari  timu nzito na zenye wachezaji tajika kama vile wenyeji  Misri ,Mali ,Ghana Morocco  na Cameroun  zimeonyesha mlango kutoka mashindano hayo .Je unafikiri  timu gani mbili zitatamba leo kati ya  Ivory Coast dhidi ya Algeria na  Madagascar dhidi ya Tunisia?

View Comments