Timu tano za kuangazia msimu ujao ligi kuu Uhispania
Laliga Santander inatarajiwa kung'oa nang'a hii leo huku mechi ya kwanza ikiwa baina ya bingwa mtetezi Barcelona dhidi ya Athletic Bilbao.
Kwa muda sasa klabu ya Barcelona imekuwa ikitawala ligi hio huku Lionel Messi akiwakosesha usingizi mabeki pamoja na walinda lango wa timu pinzani. Hata hivyo, Vilabu vingine vimekuwa na biashara za kufana sana na huenda vikaletea mabingwa hao wakati mgumu msimu huu.
Atletico Madrid
Real Madrid
Zinedine Zidane amemsajili kiungo mshambulizi wa Chelsea, Eden Hazard ili aweze kumsaidia kungangania taji la ligi kuu nchini Uhispania.
Hazard anatarajiwa kurudisha furaha mioyoni mwa wapenzi wa klabu ya Real Madrid msimu huu haswa baada ya kukosekanana mfungaji wa kutegemewa msimu uliopita.
Zidane amefanya sajili nne kufikia sasa na huenda akamsajili Neymar kabla dirisha la Uhamisho halijakamilika.
Villareal
\
Barcelona
Mkurugezi mkuu wa Barcelona Josep Martina aliweka wazi matamanio ya kuona klabu yake ikimaliza msimu kama haijapoteza mchezo hata mmoja.
Barcelona imemsajili Antoinne Griezmann pamoja na Frankie De Jong kuongeza kwenye kikosi cha Barcelona. Msimu uliopita Barcelona ilipoteza michuano mitatu pekee na sasa wanaazimia kuimarisha rekodi hio. Je wataweza?
Sevilla
Sevilla imemleta aliyekuwa kocha wa timu ya taifa ya Uhispania, Julen Lopetegui na sasa anatarajiwa kuleta ushindani mkali msimu ikizingatiwa kwamba alifukuzwa kazi msimu uliopita na klabu ya Real Madrid.
Hata hivyo, Usajili wake Rony Lopez, Luuke De Jong pamoja na Olivier Torres inatarajiwa kuongeza ushindani kwenye ligi kuu Uhispania msimu ujao.