Mourinho: Mashabiki wa Arsenal, Chelsea na United watoa hisia zao
Klabu ya North London na anakochezea nahodha wa Harambee Stars, Victor Wanyama, Tottenham imemteua Jose Mourinho kama kocha mpya.
Mourinho ambaye awali alikuwa mkufunzi wa Chelsea na pia Manchester United kwenye ligi kuu ya Uingereza, anajiunga na Spurs masaa machache tu baada ya kutimuliwa kwake Mauricio Pochettino.
Pochettino alifutwa kazi jana baada ya miaka mitano ya kuingoza klabu hiyo ya North London. Mourinho amekua bila ya ajira baada ya kufutwa kama meneja wa United Disemba mwaka 2018.
Pochettino aliiongoza Spurs kumaliza katika nafasi ya nne bora katika misimu minne kati ya mitano aliyokuwa meneja wa klabu hiyo na vilevile fainali yao ya kwanza la ligi ya mabingwa mwaka wa 2018/19.
Akizungumza baada ya uteuzi wake, Mourinho alisema,
Son will be a left back , Harry Kane will be the best defender in the EPL .. 😂🤣