Victor Wanyama  ametemwa kutoka kikosi cha kwanza cha totnham Hotspurs cha mechi za kombe la mabingwa baada ya kocha Jose Mournho kukiri kwamba alikuwa na wachezaji wengi  aliowazingatia mbele ya wanyama katika kikosi chake . Mourinho amesema uamuzi huo wa kumuacha nje Wanyama umetokana na ushindani mkali katika safi ya kati .Mechi za kombe hilo  zitarejelewa tena mwezi huu .

Tottenham  itachuana na  RB Leipzig  katika mkondo wa kwanza  kwenye mashindano ya 16 bora  februari tarehe 19  wakiwa nyumbani kabla ya mchuano wa mkondo wa pili mwezi ujao tarehe 10  baada ya kufika fainali mwaka uliopita .

Sheria za UEFA zinairuhusu timu kukifanyia mageuzi kikosi chake  kabla ya awamu ya maondoano  na Mourinho ameitumia fursa hiyo kumtema Wanyama ,nahodha wa kikosi cha Harambee Stars  lakini akaamuakusalia na walinda lago watano katika kikosi cha wachezaji 30.

View Comments