In Summary
  • Shirikisho la Soka la Uhispania (RFEF) lilisema: "RFEF na Bw Rais wataonyesha kila moja ya uwongo unaoenezwa na mtu kwa niaba ya mchezaji au, ikiwezekana, na mchezaji mwenyewe.
Rais wa FA Uhispania akosolewa kwa kumpiga busu mchezaji
Image: BBC

Shirikisho la soka la Uhispania linasema litachukua hatua za kisheria kuhusu maoni ya Jenni Hermoso kuhusu rais wake Luis Rubiales.

Rubiales amekataa kujiuzulu baada ya kumbusu fowadi Hermoso kwenye midomo kufuatia ushindi wa fainali ya Kombe la Dunia la Wanawake wa Uhispania dhidi ya England mjini Sydney.

Hermoso alisema mnamo Ijumaa hakukubali, lakini shirikisho limehoji toleo lake la matukio.

"Ushahidi ni muadilifu," ilisema. "Mheshimiwa Rais hajadanganya."

Katika taarifa ya chama cha wachezaji cha Futpro, ambacho kinamwakilisha Hermoso mwenye umri wa miaka 33, alinukuliwa akisema "hakuna mahala ambapo nilitaka kumuinua (kumwinua) rais" wakati wakikumbatiana kwenye jukwaa.

Shirikisho la Soka la Uhispania (RFEF) lilisema: "RFEF na Bw Rais wataonyesha kila moja ya uwongo unaoenezwa na mtu kwa niaba ya mchezaji au, ikiwezekana, na mchezaji mwenyewe.

"RFEF na Rais, kwa kuzingatia uzito wa maudhui ya taarifa kwa vyombo vya habari kutoka kwa muungano wa Futpro, wataanzisha hatua zinazolingana za kisheria."

Shirikisho hilo pia lilisema kwamba, wanapochaguliwa, wachezaji wana "wajibu" wa kuichezea timu ya taifa, baada ya wachezaji 81 wa kike kusema hawataiwakilisha Uhispania hadi Rubiales aondolewe kwenye wadhifa wake.

Mshambulizi wa Real Betis, Borja Iglesias pia amesema hataichezea tena timu ya taifa ya wanaume huku Rubiales akiwa msimamizi wa shirikisho hilo.

Katika taarifa yake, RFEF ilitoa picha nne za kukumbatiana kwa Hermoso na Rubiales, na uchambuzi wa kila moja, ambao inadai inaonyesha kuwa alitumia nguvu kuinua miguu ya Rubiales kutoka ardhini.

Shirikisho hilo linasema limejaribu kuwasiliana na Hermoso, ambaye ndiye mfungaji bora wa mabao wa Uhispania kwa wanawake akiwa na mabao 51 kati ya mechi 101, lakini "haijafanikiwa kila wakati".

 

 

 

 

 

 

 

View Comments