In Summary

•Cena alitoa tangazo hilo ambalo halikutarajiwa na mashabiki zake wakati wa kuonekana kwenye hafla ya WWE Money in the Bank nchini Canada.

•Mchezaji huyo alisema shindano lake la mwisho kuingia ulingoni litakuwa 2025 kama sehemu ya ziara ya kuaga.

John Cena//Instagram

Muigizaji na mwanamieleka wa Marekani John Cena ametangaza kustaafu kushiriki mashindano ya World Wrestling Entertainment (WWE).

Cena alitoa tangazo hilo ambalo halikutarajiwa na mashabiki zake wakati wa kuonekana kwenye hafla ya WWE Money in the Bank nchini Canada.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 47, ambaye aliingia katika uigizaji miaka 18 iliyopita, alisema shindano lake la mwisho kuingia ulingoni litakuwa 2025 kama sehemu ya ziara ya kuaga.

Cena mara nyingi anachukuliwa kuwa mmoja wa wanamieleka wa kitaalamu zaidi wa wakati wote na alipata hadhi ya bingwa wa dunia mara 16 tangu ajiunge na WWE mnamo 2001.

"Leo usiku natangaza rasmi kustaafu kwangu kutoka kwa WWE," aliwaambia mashabiki wa Toronto ambao walijibu kwa mshangao na baadaye kuimba "asante Cena".

"Ni ishara ya kipekee ya wema," alijibu.

Akiwa amevalia fulana yenye maandishi "Wakati wa Mwisho ni Sasa" na nembo yake ya "jorts" [kaptura ya denim], aliwashukuru mashabiki wa WWE kwa "kuniruhusu kucheza kwenye nyumba ambayo mmeijenga kwa miaka mingi".

Katika mkutano na waandishi wa habari baadaye, alisema ana nia ya kubaki sehemu ya familia ya WWE katika nafasi fulani licha ya kuhisi "mwisho wangu" kimwili.

Cena alianza kuigiza kwa mara ya kwanza mwaka wa 2006 katika filamu ya The Marine, akaendelea na majukumu katika filamu kadhaa kubwa zikiwemo The Suicide Squad, Fast & Furious 9 na Teenage Mutant Ninja Turtles.

Nyota huyo amecheza kwa muda katika WWE tangu 2018 wakati taaluma yake ya uigizaji ilipoanza.

Aligonga vichwa vya habari mwaka huu baada ya kuonekana uchi, akiwa amejifunika bahasha tu kwa njia ya kimkakati, wakati wa Tuzo za Academy.

View Comments