logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mark Otieno aomba kuondolewa marufuku yake baada ya maabara kuthibitisha hakutumia dawa za kusisimua misuli

Kirutubisho alichokuwa akitumia kilikuwa kimechafuliwa kwa dawa isiyotajwa ambayo imepigwa marufuku.

image
na Radio Jambo

Makala18 March 2022 - 04:32

Muhtasari


•Otieno anataka marufuku iliyowekwa dhidi mwaka jana kuondolewa baada matokeo ya maabara kubaini kuwa hakutumia dawa za kusisimua misuli.

•Mwanariadha huyo ameeleza kwamba amekuwa akipitia kipindi kigumu katika juhudi za kusafisha jina lake na kuthibitisha kuwa hana hatia.

Bingwa wa mbio za mita 100 Mark Otieno Odhiambo ameomba kuruhusiwa kushiriki tena katika mashindano.

Otieno anataka marufuku iliyowekwa dhidi mwaka jana kuondolewa baada matokeo ya maabara kubaini kuwa hakutumia dawa za kusisimua misuli.

Kupitia taarifa, Mwanariadha huyo amesema kuwa matokeo ya maabara ambayo alipokea miezi kadhaa iliyopita yaliashiria kuwa kirutubisho alichokuwa akitumia kilikuwa kimechafuliwa kwa dawa isiyotajwa ambayo imepigwa marufuku.

"Miezi kadhaa iliyopita nilipokea matokeo kutoka kwa maabara iliyopitishwa na WADA yakithibitisha mashaka yangu kwamba mojawapo ya virutubisho vya lishe ambavyo nilikuwa natumia vilichafuliwa kwa kitu kilichopigwa marufuku ambacho kilisababisha kipimo + kwenye Olimpiki za Tokyo. Matokeo haya yanathibitisha bila shaka kwamba sikutumia madawa ya kusisimua misuli kama ambavyo nimekuwa nikisisitiza tangu mwanzo," Otieno amesema.

Mwanariadha huyo ameeleza kwamba amekuwa akipitia kipindi kigumu katika juhudi za kusafisha jina lake na kuthibitisha kuwa hana hatia.

Amesema kuwa tayari ameandika barua kwa wahusika wote akiomba marufuku aliyowekewa iondolewe ili aruhusiwe kukimbia tena.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved