logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Hongera!Hellen Obiri ashinda mbio za Boston Marathon kwa wanawake

Bingwa huyo wa mbio za mita 5,000 alikata mkanda huo kwa muda wa 2:21:38.

image
na Radio Jambo

Makala17 April 2023 - 16:24

Muhtasari


  • Chebet alikuwa akitetea ushindi wake katika Marathon ya wanaume baada ya kushinda mwaka jana.

Mwanariadha wa Kenya Hellen Obiri ameshinda mbio za Boston Marathon.

Bingwa huyo wa mbio za mita 5,000 alikata mkanda huo kwa muda wa 2:21:38.

Obiri alicheza marathon kwa mara ya kwanza mwaka jana alipokimbia New York City Marathon ambapo alishika nafasi ya sita.

Ushindi wake unakuja baada ya Evans Chebet kutetea vyema taji lake la Boston Marathon mnamo Aprili 17, baada ya kutumia muda wa 2:05:54.

Chebet alikuwa akitetea ushindi wake katika Marathon ya wanaume baada ya kushinda mwaka jana.

Geoffrey Mutai anashikilia rekodi ya kozi ya Boston Marathon ya 2:03:02 kutoka 2011.

Zawadi ya fedha taslimu ya mshindi kwa wanaume na wanawake imepangwa kuwa dola 150,000 ambazo ni sawa na Sh20 milioni.

Kwa mshindi wa Medali ya Fedha, ambayo ni nafasi ya pili, washindi watachukua hadi dola 75,000 sawa na Sh10 milioni.

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved