logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Arsenal yatozwa faini ya Sh3M kwa kukosa kudhibiti wachezaji wake

Klabu hiyo ya London imekiri makosa yake na kukubali adhabu ya kutoa faini ya pauni 20,000 kama ilivyopendekezwa.

image
na Radio Jambo

Habari06 January 2022 - 10:37

Muhtasari


•Klabu hiyo ya London imekiri makosa yake na kukubali adhabu ya kutoa faini ya pauni 20,000 kama ilivyopendekezwa.

Shirikisho la soka (FA|) limetoza klabu ya Arsenal pauni 20,000 (Ksh 3M) baada ya kukabili kosa la kukosa kudhibiti wachezaji wake katika mechi dhidi ya Mancheter City siku ya Jumamosi.

FA ilikuwa imepatia Wanabunduki hadi Ijumaa kujibu mashtaka ya kushindwa kuhakikisha wachezaji wao wanajiendesha kwa utaratibu ufaao wakati wa mechi hiyo iliyochezwa ugani Emirates.

Tukio hilo lilitokea dakika ya 59 baada ya beki wa Gunners, Gabriel Magalhaes kutolewa nje kwa kadi nyekundu baada ya kupokea kadi ya pili ya njano.

Kufuatia hayo klabu hiyo ya London imekiri makosa yake na kukubali adhabu ya kutoa faini ya pauni 20,000 kama ilivyopendekezwa.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved