logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Ni muujiza kurejea katika soka-Christian Eriksen

Eriksen amefungwa kifaa cha maalum cha kuwezesha moyo wake kupiga

image
na Radio Jambo

Yanayojiri12 February 2022 - 12:02

Muhtasari


•Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 29 amefungwa kifaa cha maalum cha kuwezesha moyo wake kupiga cardioverter-defibrillator (ICD), baada ya kupatwa na mshtuko wa moyo.

Christian Eriksen asajiliwa na Brentford

Christian Eriksen anasema ni muujiza kuweza kuanza tena soka akiwa na Brentford baada ya kuzimia alipokuwa akiichezea Denmark kwenye Euro 2020 msimu uliopita wa joto.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 29 amefungwa kifaa cha maalum cha kuwezesha moyo wake kupiga cardioverter-defibrillator (ICD), baada ya kupatwa na mshtuko wa moyo.

Amejiunga na The Bees kwa mkataba wa miezi sita baada ya kuachiliwa na Inter Milan.

"Jambo la kwanza ni kuonesha shukrani," Eriksen aliiambia BBC Sport. "Kwa watu wanaonizunguka, wachezaji wenzangu, madaktari kwanza uwanjani, madaktari wa timu na wahudumu wa afya na kisha hospitalini, kufanya kila kitu na kuangalia kila kitu.

"Halafu ujumbe wote kutoka kwa watu kwa kuniunga mkono kwa yale ambayo familia yangu imepitia.

Imekuwa vizuri sana kuona ujumbe wa shukrani. "Nina bahati sana na nimewaambia ana kwa ana, nimefurahi sana wamefanya walichofanya vinginevyo nisingekuwa hapa."


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved