logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Rasmi! Mshambuliaji Erling Haaland kujiunga na Manchester City

Makubaliano ya masharti kati ya klabu na Halaand bado yanaendelea.

image
na Radio Jambo

Makala11 May 2022 - 02:17

Muhtasari


•Jumanne jioni mabingwa hao wa EPL mara tano walitanganza kuwa Halaand atakuwa anajiunga nao rasmi mnamo Julai 1, 2022.

•Manchester City imetangaza kuwa makubaliano ya masharti kati ya klabu na Halaand bado yanaendelea.

Washambulizi Erling Haaland na Phil Foden

Klabu ya Manchester City imeafikia makubaliano na Borussia Dortmund kwa uhamisho wa mshambuliaji matata Erling Halaand.

Jumanne jioni mabingwa hao wa EPL mara tano walitanganza kuwa Halaand atakuwa anajiunga nao rasmi mnamo Julai 1, 2022.

"Manchester City inaweza kuthibitisha kwamba tumefikia makubaliano kimsingi na Borrusia Dortmund kwa uhamisho wa mshambuliaji Erling Halaand kujiunga na klabu tarehe 1 Julai 2022," City ilitangaza kupitia tovuti rasmi ya klabu.

Mabingwa hao watetezi wa ligi ya Premier wametangaza kuwa makubaliano ya masharti kati ya klabu na Halaand bado yanaendelea.

City inatarajiwa kulipa Dortmund ada isiyopungukia Euro milioni 60. Haaland atakuwa miongoni mwa wachezaji wanaopokea mshahara mkubwa zaidi huku akilipwa takriban pauni 375, 000 kwa wiki.

Premier League imemkaribisha mzaliwa huyo wa Norway ambaye tayari ameonyesha umahiri mkubwa wa soka licha ya kuwa na miaka 21 tu.

Kufikia sasa Haaland ndiye mfungaji bora wa tatu katika Bundesliga huku akiwa amefunga mabao 21 na kusaidia katika mabao 7.

Mshambulizi huyo ndiye mfungaji bora wa Dortmund tangu alipojiunga nao takriban miaka miwili iliyopita.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved