logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Simba yavunja mkataba na kocha wake Mkuu

Vile vile Klabu ya Simba imefikia makubaliano ya pande mbili ya kuvunja mkataba

image
na Radio Jambo

Makala31 May 2022 - 12:52

Muhtasari


  • Vile vile Klabu ya Simba imefikia makubaliano ya pande mbili ya kuvunja mkataba na kocha wa viungo Daniel De Castro Reyes

Klabu ya Simba imefikia makubaliano ya pande zote mbii ya kuvunja mkataba na Kocha Mkuu wa timu hiyo Pablo Franco Martin.

Katika kipindi chake Kocha Pablo ameiwezesha timu yetu kutwaa ubingwa wa kombe la Mapinduzi na kufika robo fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika.

Uongozi wa Klabu ya Simba umeandika taarifa yake na kumshukuru Kocha Pablo kwa mchango wake ndani ya klabu hiyo.

‘’Katika kipindi chote cha kumaliza msimu kikosi chetu kitakua chini ya Kocha Msaidizi Selemani Matola’’ Ilisema sehemu ya taarifa hiyo.

Vile vile Klabu ya Simba imefikia makubaliano ya pande mbili ya kuvunja mkataba na kocha wa viungo Daniel De Castro Reyes.

 

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved