In Summary

• Mwanaspoti huyo, 23, alivalia suti ya hudhurungi iliyompwerepweta ambayo aliiunganisha na jozi ya viatu vilivyofanana na suti hiyo.

Kiungo wa kati wa Chelsea
Image: Instagram

Kiungo wa kati wa Chelsea, Mason Mount amefanya mashabiki wazungumze, baada ya kuvaa mavazi ya ukubwa kupita kiasi kwenye onyesho la kwanza la Black Panther: Wakanda Forever mnamo Alhamisi, Novemba 3.

Mount alikuwa akiichezea Chelsea usiku uliotangulia kwenye mpambano wao wa Ligi ya Mabingwa dhidi ya Dinamo Zagreb. The Blues walishinda mchezo huo kwa mabao 2-1 na Mount akashinda tuzo ya mchezaji bora wa mechi.

Mwanaspoti huyo, 23, alivalia suti ya hudhurungi iliyompwerepweta ambayo aliiunganisha na jozi ya viatu vilivyofanana na suti hiyo.

Alivalia fulana nyeupe na kujiweka sawa huku mikono yake ikiwa mfukoni, baada ya kuthibitisha kutengana kwake na mpenzi wake mwanamitindo Chloe Wealleans-Watts baada ya miaka mitano pamoja mwezi uliopita.

Filamu hiyo iliyoasiliwa na kampuni ya Marvel, ambayo pia iliongozwa na Ryan Coogler, imekuwa mojawapo ya filamu zilizoingiza pesa nyingi zaidi wakati wote.

Wakati huo, ilikuwa filamu ya kwanza tangu Avatar - filamu iliyoingiza pesa nyingi zaidi - kuongoza kwenye chati kwa wikendi tano mfululizo.

Katika filamu ya asili, mwigizaji marehemu, Chadwick Boseman, ambaye aliaga dunia mwaka wa 2020, aliigiza kama mhusika mkuu na jina la Black Panther, huku kukiwa na wasanii waliojumuisha pia Michael B. Jordan na mshindi wa Oscar Lupita Nyong'o.

Muonekano huo wa Mount uliwashangaza wengi huku baadhi wakiibua kumbu kumbu kuwa msanii Justine Bieber pia aliwahi tokea na muonekano wa nguo kubwa katika tuzo za kifahari mapema mwaka huu.

View Comments