logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Cristiano Ronaldo:Nimeimaliza kazi yangu Ulaya

Ronaldo alisema alikuwa na ofa kutoka kwa vilabu vya Brazil, Australia, Marekani na Ureno.

image
na Radio Jambo

Habari04 January 2023 - 06:52

Muhtasari


•Alijiunga na Al Nassr baada ya kuondoka Manchester United kufuatia mahojiano yenye utata ambapo aliikosoa klabu hiyo.

Cristiano Ronaldo anasema kazi yake barani Ulaya imekamilika, lakini alikuwa na "nafasi nyingi" kutoka kwa vilabu vingine kabla ya kujiunga na Al Nassr ya Saudi Arabia.

Alijiunga na Al Nassr kama mchezaji huru siku ya Ijumaa baada ya kuondoka Manchester United kufuatia mahojiano yenye utata ambapo aliikosoa klabu hiyo.

Nahodha huyo wa Ureno, 37, alisema alikuwa na ofa kutoka kwa vilabu vya Brazil, Australia, Marekani na Ureno.

"Nilitoa ahadi yangu kwa klabu hii," alisema wakati wa uzinduzi wake Jumanne.

"Nilishinda kila kitu, nilichezea vilabu muhimu zaidi barani Ulaya na sasa ni changamoto mpya barani Asia."

Ronaldo anaripotiwa kupokea mshahara mkubwa zaidi katika historia ya soka wa zaidi ya £177m kwa mwaka katika mkataba unaoendelea hadi 2025.

"Kama hakuna anayejua, naweza kusema sasa nilikuwa na fursa nyingi Ulaya, vilabu vingi nchini Brazil, Australia, Marekani, hata Ureno, vilabu vingi vilijaribu kunisajili," Ronaldo aliwaambia waandishi wa habari katika mkutano wake wa kwanza na wanahabari.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved