logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Man U yaibuka timu bora na yenye thamani kubwa katika ligi kuu ya Premia

Mara ya mwisho kwa Man U kushindwa ubingwa wa Premia ilikuwa mwaka 2013.

image
na Radio Jambo

Makala25 January 2023 - 09:36

Muhtasari


• United kwa sasa ndio timu pekee kutoka Uongereza iliyosalia katika mashindano ya mataji 4 tofuati.

• United inafukuzia ubingwa wa Premia, ligi ya Uropa, kombe la FA na ngao ya Carabao.

Manchester United

Kwa mara nyingine tena, timu ya soka ya Manchester United imeibuka kidedea kama timu yenye thamani kubwa zaidi katika ligi kuu ya Premia nchini Uingereza.

Katika orodha ambayo imetolewa hivi karibuni, Manchester United wametajwa kama timu yenye thamani kubwa zaidi na kuwabwaga wapinzani wao wa karibu kama Mabingwa watetezi wa taji la Premia Manchester City, watani wa jadi Arsenal na wababe Liverpool.

Hili linakuja licha ya timu hiyo kukaa bila kushinda ligi ya Premia kwa miaka 10 sasa tangu kufanya hivo mara ya mwisho wakiwa na kocha mstaafu Sir Alex Ferguson mwaka 2013.

United wanazidi kufurahia mwenendo mzuri uwanjani msimu huu chini ya Erik ten Hag, ambaye alijiunga na klabu hiyo msimu wa joto kuchukua nafasi ya Ralf Rangnick.

Ndio timu ya pekee kutoka Uingereza ambayo imesalia katika mashindano ya mataji zaidi ya matatu yakiwemo ubingwa wa ligi ya Uropa, ligi kuu ya Premia, taji la FA na ngao ya Carabao mtawalia.

Kulingana na jarida la Sportico, United ina thamani ya pauni bilioni 4.8 huku Liverpool wakiwanyemelea kwa ukaribu kwa thamani ya pauni bilioni 3.8.

Orodha hiyo inaendelea kwa timu ya Manchester City yenye thamani ya pauni bilioni 3.5, Arsenal wanafunga nne bora kwa utajiri wa pauni bilioni 2.9.

Chelsea wanaikaribia Arsenal katika nafasi ya tano na utajiri wa pauni bilioni 2.8 huku Tottnham Hotspurs Tottenham pauni bilioni 2.6, West Ham wakiwa na thamani ya pauni milioni 539, Everton pauni milioni 486, Leicester pauni milioni 442, na Newcastle wakihitimisha kumi bora kwa utajiri wa pauni milioni 357.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved