logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Instastory yasababisha kuvunjika kwa uhusiano wa Gabriel Jesus na mpenzi wake

Raiane Lima anadaiwa kuandika ujumbe wa kutengana na Jesus kwenye Instagram na kuufuta.

image
na Radio Jambo

Makala26 January 2023 - 13:04

Muhtasari


• Inaarifiwa kuwa Raiane Lima aliandika ujumbe wa kuvinja uchumba kwenye Instagram yake na kuufuta dakika kadhaa baadae.

• Wawili hao wamekuwa pamoja tangu mwaka 2021 na miezi 8 iliyopita walibarikiwa na mtoto wa kike kwa jina Helena.

Gabriel Jesus adaiwa kuachwa na mpenzi wake Raiane Lima

Mshambuliaji wa Arsenal Mbrazil Gabriel Jesus ameripotiwa kuachwa na mpenzi wake Riaine Lima miezi minane tu baada ya wachumba hao wachanga kukaribisha mtoto wao.

Kulingana na jarida la The Sun la nchini Uingereza, Ripoti nchini Brazil ziliibuka kuwa mshawishi wa mitandao ya kijamii Raiane, 21, alitangaza kuwa ametengana na nyota huyo wa Arsenal, 25, kufuatia hadithi inayodaiwa kuwa kwenye Instagram (Instastory).

Jarida hilo pia lilizidi kufichua kuwa Chombo cha UOL cha Brazil kinadai Raiane alitumia Instagram story yake kuthibitisha habari hizo, lakini chapisho lake halipatikani tena.

Anadaiwa kuandika kwenye instastory yake: "Kabla ya uvumi kuenea, mimi mwenyewe hufanya hatua ya kukujulisha kuwa mimi na Gabriel sio wanandoa tena. Na yeyote anayetaka kuhukumu anaweza kuhukumu. Yeyote anayetaka kusema mambo mabaya anaweza kusema. Kwa kuwa wengine wanapenda fedheha, mimi hufanya hivyo mwenyewe swali la kutangaza mwisho wa kitu ambacho karibu kunimaliza. Nani anataka kusherehekea pia, anaweza kusherehekea (hasa wanafamilia).”

"Baada ya chapisho hili, unajua kuwa hautaniona tena nikizungumza juu ya tuliyopitia, au juu ya somo lolote linalohusiana na binti yetu. Haukuwa usaliti, ilikuwa shinikizo kutoka kwa kila mtu na kila kitu. Tuliishi vizuri, lakini kwa sababu ya shida za watu wengine, kila wakati ilitupata. Siwezi kuvumilia tena, na sitajilazimisha kufanya kitu ambacho kinaniua,” The Sun walinukuu instastory hiyo ambayo ilifutwa baada ya muda mfupi.

Inakuja miezi minane tu baada ya Raiane kujifungua mtoto wao wa kike, Helena. Hakuna picha za Jesus na Raiane wakiwa pamoja kwenye ukurasa wake wa Instagram, kwani inaaminika ameshazifuta zote.

Wapenzi hao wachanga Wanaripotiwa kuwa pamoja tangu Julai 2021.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved