logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Beki wa Liverpool aomba radhi kwa mashabiki baada ya kudhalilishwa na Brighton

" Ninawahurumia mashabiki. Walikuwa wa ajabu leo ​​na tumewaangusha tena,”

image
na Radio Jambo

Makala30 January 2023 - 11:06

Muhtasari


• Liverpool amabo ni mabingwa watetezi wa kombe la FA walitupwa nje na Brighton kwa ushinde wa mabao 2-1.

Liverpool waomba mashabiki wao msamaha kwa kudhalilishwa na Brighton

Beki wa Liverpool, Andy Robertson amekiri kuwa Liverpool "haijakaribia ubora wao wa kawaida vya kutosha" huku mabingwa hao wa Kombe la FA wakibanduliwa nje ya FA na Brighton Jumapili.

Mshangao wa dakika za majeruhi wa Kaoru Mitoma ulifikisha ukomo wa kampeni ya Reds ya kutaka kutwaa kombe hilo kwa mara nyingine tena huku kikosi cha Jurgen Klopp kikipokezwa kichapo cha pili mtawalia na Brighton ndani ya siku 15.

Kulingana na beki huyo ambaye aliomba radhi kwa mashabiki wa klabu hiyo, alisema: "Msimu huu haujatukubali vya kutosha. Tulitaka mwanzo mpya mwanzoni mwa mwaka. Ikiwa chochote, tumekuwa mbaya zaidi. Huwezi kuweka kidole chako kwenye jambo moja ambalo limeharibika, ni zaidi ya hilo. Unaweza kusema kwamba hatujiamini mbele ya lango; bado tuko duni kwa kujilinda. Tunahitaji kurudisha imani yetu. Ninawahurumia mashabiki. Walikuwa wa ajabu leo ​​na tumewaangusha tena,” The Sun walimnukuu.

Liverpool walichukua uongozi katika nusu saa kupitia kwa Harvey Elliott lakini wakabanwa na Lewis Dunk, kabla ya Mitoma kuwahakikishia ushindi dakika za majeruhi kwa udhibiti na utulivu.

Maneno makali ya Robertson yaliwekwa kwa Klopp na Mjerumani huyo akajibu: "Sio ukweli kwa asilimia 100, lakini sio makosa kwa asilimia 100. Bila shaka unataka mwanzo mpya unaporudi baada ya mapumziko ya Kombe la Dunia, unataka kwenda hiyo.”

Mitoma alisajiliwa kwa Pauni Milioni 2.5 tu kutoka Kawasaki Frontale ya Japan mwaka 2021, kabla ya kwenda kwa mkopo katika klabu ya Albion ya Ubelgiji, Union Saint-Gilloise msimu uliopita.

Amekuwa kificho msimu huu, akifunga mabao sita katika mechi 19 akiwa na Seagulls,

Liverpool waomba mashabiki wao msamaha kwa kudhalilishwa na Brighton

RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved