logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Aboubakar: Ronaldo alijaribu kunizuia nisiondoke klabu ya Saudi

"Tulizungumza kidogo na Cristiano aliniambia kwamba ni vyema nibaki ila nilimwambia hapana,

image
na Radio Jambo

Makala15 February 2023 - 12:20

Muhtasari


  • Licha ya nyota huyo wa zamani wa Man United na Real Madrid kujaribu kumzuia kuondoka, Aboubakar aliamua kurejea Besiktas ya Uturuki

Nahodha wa Cameroon Vincent Aboubakar amesema Cristiano Ronaldo alijaribu kuzungumza naye ili aachane na Al Nassr, baada ya nyota huyo wa Ureno kuwasili katika klabu hiyo ya Saudia.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 31, ambaye alikuwa amebaki na miezi sita katika mkataba wake wa Al Nassr, alijua kabisa kwamba mchezaji wa kigeni angelazimika kutolewa kwa ajili ya mshindi huyo mara tano wa tuzo ya Ballon d'Or.

Licha ya nyota huyo wa zamani wa Man United na Real Madrid kujaribu kumzuia kuondoka, Aboubakar aliamua kurejea Besiktas ya Uturuki kwa kusaini miaka miwili na nusu mnamo mwezi Januari.

"Tulizungumza kidogo na Cristiano aliniambia kwamba ni vyema nibaki ila nilimwambia hapana, na kwamba nitaondoka kwa sababu za kifamilia," Aboubakar aliiambia Talents d'Afrique kwenye Canal+.

“Aliniuliza familia yangu iko wapi, nikamwambia iko Ufaransa lakini napendelea kwenda Uturuki, ni karibu zaidi.

"Na aliniambia ni bora, ikiwa familia iko mbali sana, ni ngumu zaidi.

Kwa kuwa nilikuwa nataka kuondoka tu."

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved