logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Neymar aapa kurejea PSG akiwa kwa kishindo zaidi

Mchezaji wa PSG kutoka Brazil,Neymar ameapa kurjea PSG na nguvu zaidi.

image
na

Makala07 March 2023 - 05:12

Muhtasari


Paris Saint Germain  ilidhibitisha kuwa Neymar anahitaji upasuaji wa kiundo cha mguu na atakuwa nje ya uwanja kwa muda wa miezi tatu au minne

Mchezaji kutoka Brazil,Neymar ambaye anachezea timu ya PSG ,aliahidi kurejea mwenye nguvu zaidi.Hii ni baada ya mchezaji huyo  kuumia kifundo cha mguu mnamo Februari 19 dhidi ya Lille kwenye Ligue 1. Klabu hiyo ilisema kuwa madaktari wake walipendekeza upasuaji wa kurekebisha ligament ili kurekebisha tukio hilo kujirudia .

Timu hiyo iliongeza kuwa Neymar atakuwa nje ya uwanja kwa miezi mitatu hadi minne hivyo uwezekano wa yeye  kuwa kwenye ligi  msimu hii ni kidogo sana kwa sababu  mwisho wa msimu huu utakuwa Juni 3.

"Nitarudi na nguvu zaidi,"alichapisha kwenye mtandao wa Twitter.

Neymar ambaye amefunga mabao 18 katika michuano yote kwa klabu ya msimu huu, alikuwa katika kiwango kizuri kwa mabingwa hao wa Ufaransa kabla ya mapumziko ya Kombe la Dunia .

Lakini mchezaji huyo wa miaka 31 ametikisa nyavu mara tatu pekee katika mechi tisa tangu arejee kutoka Qatar,ambako aliumia kifundo cha mguu akiichezea Brazil.Mchezaji huyo wa zamani wa Barcelona alirejea katika raundi ya mtoano lakini Brazil wakshindwa na Croatia kwa mikwaju ya penalti katika robo fainali,licha ya Neymar kuwaweka mbele katika  muda wa ziada katika mchezo huu.

Neymar ameweka mabao 118 katika michezo 173 kule aPSG lakini alikosa zaidi ya michezo 100 kwa sababu ya kuumia .Katika Ligue 1 amecheza asilimia 49 pekee ya mechi za PSG ya Ligue 1(112 kati ya 228)


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved