logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Hali ya kutia huruma mcheza aliyegeuka kichaa akichakura mapipa ya taka kutafuta chakula

Familia ilisema kwamba mchezaji huyo anakumbwa na matatizo ya afya ya akili.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri17 March 2023 - 09:51

Muhtasari


• Mchezaji huyo amekuwa akitoweka mara kwa mara kutoka nyumbani na kutafutwa kuwekwa chini ya ulinzi wa familia.

• Wiki jana aliripotiwa kutoweka na baadae picha zake zikasambaa akila chakula cha jalalani.

Khayelihle Shozi , mchezaji wa zamani wa Mamelod Sundowns.

Hisia mseto zimeibuliwa kwenye mitandao ya kijamii baada ya picha kadhaa kusambazwa zikimuonesha aliyekuwa mchezaji maarufu wa soka Afrika Kusini akiwa kama kichaa wa kula kutoka kwa mapipa ya jalalani.

Kituo cha redio ya jamii, nchini humo, kilifichua kwenye ukurasa wao wa Facebook mnamo Alhamisi, Machi 16 kwamba nyota wa zamani wa Masandawana Khayelihle Shozi, ambaye hivi karibuni alionekana hana makazi, amepatikana na kuunganishwa na familia yake. .

“Shozi mwenye shida Amepatikana! Khayelihle Shozi, ambaye wiki iliyopita alionekana akizurura katika mitaa ya Vereeniging amepatikana na ameungana na familia yake huko Pinetown, KwaZulu-Natal. Theta FM inapenda kuwashukuru wote walioshiriki na kusaidia kupatikana kwake,” ilisomeka taarifa hiyo.

 Baada ya picha zake akiwa katika hali duni akichokora pipa la taka kwa chakula kuenezwa, watu mitandaoni walichukizwa na kitendo hicho, baadhi wakisema alikuwa na matatizo ya akili.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 28 alipitia Katika timu za vijana ya Mamelod Sundowns na kupandishwa hadi timu ya wakubwa, Baadaye alipelekwa kwa mkopo Katika Vilabu vya SuperSport United, Black Leopard, TS Galaxy na Richard Bays.

 

Jarida la Zimoja lilifichua kuwa maisha ya Khayelihle Shozi yalibadilika na kuwa mabaya zaidi mnamo 2022 alipotoweka mara mbili katika klabu yake ya zamani ya soka ya Mamelodi Sundowns.

Klabu yake ya zamani ya Mamelodi Sundowns pia ilijitolea kuingilia kati katika mapambano yake na afya ya akili wakati huo.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved