In Summary
  • Akiwa na umri wa miaka 21 tu, tayari ameichezea klabu hiyo mechi 178 na ameshiriki katika mechi zote za Ligi Kuu ya Arsenal
Bukayo Saka made his Arsenal first-team in debut in November 2018
Image: BBC

Buyako Saka ametia saini mkataba mpya wa kusalia Arsenal hadi 2027, akisema klabu hiyo "ndipo sehemu sahihi ya kupiga hatua inayofuata".

Mshambuliaji huyo wa Uingereza amefunga mabao 14 kwa The Gunners msimu huu, na kutoa pasi 11 za mabao.

Akiwa na umri wa miaka 21 tu, tayari ameichezea klabu hiyo mechi 178 na ameshiriki katika mechi zote za Ligi Kuu ya Arsenal katika kipindi cha kampeni mbili zilizopita.

“Nimefurahi sana tu,” alisema Saka.

"Kumekuwa na mazungumzo mengi na muda umepita, lakini niko hapa sasa. Nadhani hii ni klabu sahihi, mahali pazuri kupiga hatua inayofuata. Ni klabu nzuri - angalia tulipo.

"Kwangu mimi, ni juu ya kufikia malengo yangu binafsi - kiasi gani ninajisukuma na kudai kutoka kwangu kila mchezo, wiki baada ya wiki. Kisha nina watu wote wanaofaa karibu nami katika suala la familia, na ninapokuja kwenye mafunzo, wachezaji wenzangu, na wafanyakazi wa kiufundi.

"Nadhani nina kila kitu ninachohitaji ili kuwa mchezaji bora zaidi ninaweza kuwa, na ndiyo sababu nina furaha kubaki hapa na kuwa hapa kwa siku zijazo, kwa sababu ninaamini kuwa tunaweza kufikia mambo makubwa."

 

 

 

 

 

View Comments