In Summary

• Katika mahojiano na polisi, baadaye alieleza jinsi Kokolo alivyomchukulia 'kama kipande cha takataka' baada ya kupata 'alichotaka'.

Mchezaji wa ligi ya daraja la chini afikishwa mahakamani kwa kumbaka mrembo.
Image: Twitter

Mchezaji kandanda wa ligi ya daraja la chini nchini Uingereza, Williams Kokolo aliweka mto mdomoni mwa mwanafunzi ili kumzuia kupiga kelele alipokuwa akimbaka, mahakama imesikia, jarida la Uingereza limeripoti.

Beki huyo wa Burton Albion, 23, alifikishwa mahakamani akituhumiwa kwa makosa matatu ya ubakaji katika Mahakama ya Coventry Crown siku ya Jumatatu.

Kokolo mzaliwa wa Ufaransa anatuhumiwa kumshambulia mwanamke kijana baada ya kumwalika kwenye karamu katika kumbi za chuo kikuu chake huko Birmingham mnamo Februari 13 mwaka jana.

Mwanamke huyo mwenye umri wa miaka 24 alikutana na mchezaji huyo kwenye tovuti ya uchumba na wawili hao walikuwa wakituma ujumbe akitaka kumfahamu zaidi, mahakama iliambiwa.

Baada ya kumkaribisha tena chumbani kwake, mwanafunzi huyo alikwenda bafuni na kurudi na kumkuta Kokolo akiwa amevalia kaptura yake tu kabla ya kwenda kumbaka, mahakama ilielezwa.

Inasemekana kwamba Kokolo alimlazimisha mwanamke huyo kumfanyia ngono ya mdomo kabla ya yeye pia kufanya naye ngono huku akimsihi aache.

Mahakama ilisikia kwamba 'alichukua mto mdogo na kuulazimisha mdomoni mwake' na kuendelea kumwambia 'shush'.

Mlalamishi alisema baada ya kumaliza, Kokolo alimwona ameketi kitandani na kichwa chake mikononi mwake na kuuliza: 'Kuna nini, mtoto wa kike?'

Kisha aliondoka katika eneo la Aston jijini humo usiku na mwanamke huyo alisema baadaye aliwasiliana na polisi baada ya kumweleza mpenzi wake wa zamani kilichotokea.

Katika mahojiano na polisi, baadaye alieleza jinsi Kokolo alivyomchukulia 'kama kipande cha takataka' baada ya kupata 'alichotaka'.

Kokolo, ambaye alisajiliwa na Burton kutoka Middlesbrough Januari iliyopita, alifikishwa mahakamani akituhumiwa kwa makosa matatu ya ubakaji siku ya Jumatatu.

Kokolo, ambaye alikuwa katika safu ya vijana huko Monaco kabla ya kuhamia Sunderland inayoshiriki Ligi, alikana mashtaka matatu ya ubakaji.

 

Kesi inaendelea.

View Comments