logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Aliyekuwa kipa wa Man United, Edwin van de Sar azungumzia afya yake baada ya kutolewa ICU

Awali alilazwa katika hospitali ya Split akiwa likizoni nchini Croatia.

image
na Radio Jambo

Makala19 July 2023 - 03:32

Muhtasari


•Edwin van der Sar amevunja ukimya baada ya kutolewa katika chumba cha wagonjwa mahututi (ICU) alikokuwa amelazwa kwa siku kadhaa.

•Alichukua fursa hiyo kuwashukuru watu waliosimama naye alipokuwa amelazwa katika ICU na wale waliomtakia afueni ya haraka.

Kipa wa zamani wa Manchester United na timu ya taifa ya Uholanzi Edwin van der Sar amevunja ukimya baada ya kutolewa katika chumba cha wagonjwa mahututi (ICU) alikokuwa amelazwa kwa siku kadhaa.

Mwanasoka huyo wa zamani mwenye umri wa miaka 52 alilazwa katika hospitali moja nchini Uholanzi siku kadhaa zilizopita kufuatia kuvuja damu kwenye ubongo. Awali alilazwa katika hospitali ya Split akiwa likizoni nchini Croatia.

Katika taarifa ya siku ya Jumanne, van der Sar alisema atasalia hospitalini kwa siku kadhaa huku akiendelea kupata nafuu na kwamba anatumai kuruhusiwa kwenda nyumbani wiki ijayo.

"Nina furaha kushiriki kwamba siko tena katika chumba cha wagonjwa mahututi. Walakini, bado niko hospitalini. Natumai kurejea nyumbani wiki ijayo na kuchukua hatua inayofuata katika kupona kwangu!,” van der Sar alisema siku ya Jumanne jioni.

Aliambatanisha taarifa hiyo na picha yake na mkewe wakiwa kwenye kitanda cha hospitali. Katika picha, wote wawili walivaa tabasamu kubwa kwenye nyuso zao.

Mkurugenzi Mtendaji huyo wa zamani wa Ajax alichukua fursa hiyo kuwashukuru watu waliosimama naye alipokuwa amelazwa katika ICU na wale waliomtakia afueni ya haraka.

“Tunataka kumshukuru kila mtu kwa jumbe zote nzuri na za sapoti,” alisema kipa huyo wa zamani wa Manchester United na Ajax.

Taarifa hiyo ilikuwa mawasiliano ya kwanza ya moja kwa moja ya van der Sar tangu apatikane na damu kwenye ubongo akiwa nchini Croatia mnamo Julai 7 na kulazwa katika ICU huko. Hapo awali, mkewe na Ajax walikuwa wametoa taarifa kuhusu hali yake.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved