In Summary

• Kesi ya nidhamu ilianza wiki iliyopita, huku uamuzi ukitarajiwa baadaye mwakani.

• Sasa, gazeti la Daily Telegraph limeripoti kuwa ligi hiyo imeitaka tume huru kuweka vikwazo vikali dhidi ya klabu hiyo ya Merseyside.

Everton kupokonywa pointi
Image: Facebook

Klabu ya Everton wamejipata katika hali ngumu baada ya ripoti kudai kwamba uongozi wa ligi kuu ya premia, EPL wamependekeza timu hiyo kunyang’anywa pointi 12 kwa madai ya ufujaji wa fedha ambapo wamedaiwa kukiuka sheria za fedha.

Hii ni licha ya timu hiyo ambayo imekuwa ikisuasua katika misimu iliyopita kujizolea pointi 7 tu katika mapambano 9.

Mnamo Machi, Ligi ya Premia ilipeleka Everton kwa tume huru baada ya kukagua rekodi za kifedha za vilabu vyote vya ligi kuu kwa msimu wa 2021-22.

Ingawa malipo mahususi hayajafichuliwa, inadhaniwa kuhusishwa na suala la ushuru kuhusu mikopo ya uwanja mpya wa Everton wa Bramley Moore Dock, ambao unajengwa kwa sasa.

Kesi ya nidhamu ilianza wiki iliyopita, huku uamuzi ukitarajiwa baadaye mwakani.

Sasa, gazeti la Daily Telegraph limeripoti kuwa ligi hiyo imeitaka tume huru kuweka vikwazo vikali dhidi ya klabu hiyo ya Merseyside.

Kupunguzwa kwa pointi 12 kunaweza kusababisha matokeo ya sasa ya Everton kushuka hadi chini ya pointi tano katika jedwali la ligi ya msimu unaoendelea.

Kulingana na kanuni za faida na uendelevu wa ligi, vilabu vinaweza kupata hasara ya hadi £105m katika miaka mitatu au kukabiliwa na adhabu.

Hata hivyo, Everton iliripoti hasara ya £371.8m katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita na kukabiliwa na hasara ya kila mwaka kwa miaka mitano mfululizo, ambayo ni zaidi ya £430m wakati huu.

Hakujawa na jibu rasmi kutoka kwa klabu au Ligi Kuu kuhusu maelezo ya ripoti hiyo.

 

View Comments