In Summary

• "Ilikuwa hatua kubwa kwangu, sijawahi kutoka Manchester, hata kwa mkopo au kitu kama hicho, kwa hivyo kuhamia huko peke yangu lilikuwa jambo kubwa," alisema.

Cole Palmer
Image: Instagram

Kinda matata wa Chelsea, Cole Palmer anaamini kwamba uamuzi wake wa kusikitisha wa kuondoka katika klabu ya utotoni ya Manchester City na kujiunga na Chelsea umezaa matunda baada ya kutajwa kwenye kikosi cha Uingereza kwa mara ya kwanza.

Palmer, 21, alijiunga na The Blues kwa dili la kushtukiza la pauni milioni 42.5 msimu wa joto na kuanza maisha mazuri London kwa bao la kusawazisha dakika ya 96 dhidi ya klabu yake ya zamani siku ya Jumapili, na kufuatiwa na kuitwa kwenye kikosi cha Gareth Southgate cha England.

Mshambulizi huyo analenga kucheza mechi yake ya kwanza ya wakubwa katika mchezo wa Ijumaa dhidi ya Malta katika uwanja wa Wembley au ziara ya Kaskazini mwa Macedonia siku ya Jumatatu, wakati England inakamilisha kufuzu kwa Ubingwa wa Uropa msimu ujao.

Palmer alifichua kuwa aliwaza mfululizo kwa "siku chache" baada ya Chelsea kukaribia lakini anasema aliamua kuhama kwa ajili ya kazi yake.

"Ilikuwa hatua kubwa kwangu, sijawahi kutoka Manchester, hata kwa mkopo au kitu kama hicho, kwa hivyo kuhamia huko peke yangu lilikuwa jambo kubwa," alisema.

“Niliposhuka mara ya kwanza ilikuwa ngumu, nilikuwa nakaa hotelini lakini sasa nimetulia zaidi na ninaifurahia.”

"Ilifanyika haraka sana. Nilizungumza na mtu huko Chelsea na nilikuwa nikizungumza na baba yangu lakini sikujua la kufanya. Nilikuwa nikifikiria juu yake kwa siku kadhaa, kila dakika ya siku kisha nikafikiria. kwa kazi yangu lazima niende na kupata wakati wa kawaida wa mchezo.”

"Ulikuwa uamuzi mgumu sana. Lakini ushindani uliopo [katika City], wachezaji waliokuwepo, wachezaji ambao wangejaribu kuwasajili... sikuwa na uhakika.”

"Sidhani [kuitwa kikosini England] ilikuwa sehemu kubwa ya kuwa mkweli, sikuwa hata kufikiria kuitwa Uingereza nilipoenda Chelsea mara ya kwanza, nilitaka tu kucheza michezo zaidi na kupata fursa ya kucheza kujidhihirisha [mwenyewe]. Kuitwa ni bonasi tu,” alisema katika mahojiano na jarida la Evening Standard huko UK.

View Comments