In Summary

•Spurs watalipa pauni milioni 55 pamoja na nyongeza ya pauni milioni 10 kwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26,

Image: BBC

Tottenham Hotspurs wamemsajili mshambuliaji wa Uingereza Dominic Solanke kutoka Bournemouth kwa mkataba wa £65m.

Spurs watalipa pauni milioni 55 pamoja na nyongeza ya pauni milioni 10 kwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26, ambaye amesaini mkataba hadi 2030.

Solanke, ambaye ana mechi moja, anakuwa mchezaji wa nne kusajiliwa na Tottenham msimu huu wa joto baada ya Yang Min-hyuk, Lucas Bergvall na Archie Gray.

Kocha wa Spurs Ange Postecoglou amekuwa akipambana kuimarisha safu yake ya ushambuliaji tangu nahodha wa Uingereza Harry Kane alipoondoka kuelekea Bayern Munich msimu uliopita.

View Comments