In Summary

•Kesi ya kusikilizwa kwa mashtaka 115 dhidi ya Man City kwa madai ya kukiuka kanuni za fedha za Ligi Kuu ya Uingereza inaanza leo.

MANCESTER CITY.
Image: FACEBOOK

Kesi ya kusikilizwa kwa mashtaka 115 dhidi ya Manchester City kwa madai ya kukiuka kanuni za fedha za Ligi Kuu ya Uingereza inaanza leo.

City walishtakiwa na kupelekwa kwa tume huru mnamo Februari 2023 kufuatia uchunguzi wa miaka minne. Inadaiwa City ilikiuka sheria zake za kifedha kati ya 2009 na 2018.

City inakanusha vikali mashtaka yote na wamesema kesi yao inaungwa mkono na "ushahidi wa kina usiopingika". Ligi ya Premia inadai City ilikiuka sheria zinazohitaji klabu kutoa "taarifa sahihi za kifedha zinazotoa mtazamo wa kweli na wa haki wa hali ya kifedha ya klabu".

Maelezo haya yalihusu mapato ya klabu, ambayo yanajumuisha mapato ya udhamini na gharama za uendeshaji.

Pia imewashutumu mabingwa hao wa Ligi Kuu kwa kutotoa ushirikiano. Uchunguzi wa Ligi ya Premia ulipoanza, City ilisema madai hayo ni "uongo kabisa" na kwamba madai hayo yaliyochapishwa awali katika gazeti la Ujerumani Der Spiegel yalitokana na "udukuzi haramu na uchapishaji nje ya muktadha wa barua pepe za City".

City wameshinda mataji manane ya ligi, vikombe vingi na Ligi ya Mabingwa tangu klabu hiyo iliponunuliwa 2008 na Kundi la Abu Dhabi United. "Inaanza hivi karibuni na tunatumai itakamilika hivi karibuni," meneja wa City Pep Guardiola alisema Ijumaa. “Natarajia uamuzi huo.

View Comments