logo

NOW ON AIR

Listen in Live

IEBC yatoa makataa ya kuthibitisha mpiga kura

Wakenya pia walihimizwa kuhakikisha kuwa maelezo yao ni sahihi kabla ya tarehe ya mwisho

image
na Radio Jambo

Yanayojiri30 April 2022 - 05:30

Muhtasari


  • Wakenya pia walihimizwa kuhakikisha kuwa maelezo yao ni sahihi kabla ya tarehe ya mwisho
Mwenyekiti wa IEBC Wafula Chebukati

Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) imeweka Juni 2 kuwa makataa ya kuthibitishwa kwa wapigakura kabla ya uchaguzi wa Agosti 9.

Katika taarifa iliyotolewa na baraza la uchaguzi mnamo Ijumaa, Aprili 29, bodi ya uchaguzi ilisema kuwa zoezi hilo litaanza Mei 4 na kudumu kwa muda wa mwezi mmoja.

Tume hiyo iliwataka Wakenya kuthibitisha maelezo yao ili kuhakikisha kwamba hakuna yeyote atakayefungiwa nje ya zoezi la Uchaguzi Mkuu wa Agosti.

Zaidi ya hayo, timu inayoongozwa na mwenyekiti, Wafula Chebukati ilitoa maelekezo ya jinsi zoezi hilo litakavyoendeshwa.

"Tembelea kituo chako cha usajili au afisi ya IEBC katika Eneo Bunge lako ukiwa na kitambulisho chako halisi au pasipoti halali uliyotumia kujiandikisha kama mpiga kura," ilisoma taarifa hiyo kwa sehemu.

Wakenya pia walihimizwa kuhakikisha kuwa maelezo yao ni sahihi kabla ya tarehe ya mwisho ya Juni 2 ili kuepusha msukumo wa dakika za mwisho.

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved