In Summary
  • Wakenya pia walihimizwa kuhakikisha kuwa maelezo yao ni sahihi kabla ya tarehe ya mwisho
Mwenyekiti wa IEBC Wafula Chebukati Mwenyekiti wa IEBC Wafula Chebukati

Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) imeweka Juni 2 kuwa makataa ya kuthibitishwa kwa wapigakura kabla ya uchaguzi wa Agosti 9.

Katika taarifa iliyotolewa na baraza la uchaguzi mnamo Ijumaa, Aprili 29, bodi ya uchaguzi ilisema kuwa zoezi hilo litaanza Mei 4 na kudumu kwa muda wa mwezi mmoja.

Tume hiyo iliwataka Wakenya kuthibitisha maelezo yao ili kuhakikisha kwamba hakuna yeyote atakayefungiwa nje ya zoezi la Uchaguzi Mkuu wa Agosti.

Zaidi ya hayo, timu inayoongozwa na mwenyekiti, Wafula Chebukati ilitoa maelekezo ya jinsi zoezi hilo litakavyoendeshwa.

"Tembelea kituo chako cha usajili au afisi ya IEBC katika Eneo Bunge lako ukiwa na kitambulisho chako halisi au pasipoti halali uliyotumia kujiandikisha kama mpiga kura," ilisoma taarifa hiyo kwa sehemu.

Wakenya pia walihimizwa kuhakikisha kuwa maelezo yao ni sahihi kabla ya tarehe ya mwisho ya Juni 2 ili kuepusha msukumo wa dakika za mwisho.

 

 

 

 

View Comments