logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Ngilu hatatetea kiti chake cha ugavana,Raila asema

Kinara wa ODM Raila Odinga anasema Ngilu atapewa nafasi katika utawala wake.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri15 June 2022 - 12:02

Muhtasari


  • Raila aliwataka wakazi wa Kitui katika ziara ya kampeni kuchagua kati ya David Musila wa Jubilee na Julius Malombe wa Wiper

Gavana wa Kitui Charity Ngilu hatatetea kiti chake mnamo Agosti 9.

Kinara wa ODM Raila Odinga anasema Ngilu atapewa nafasi katika utawala wake.

Raila aliwataka wakazi wa Kitui katika ziara ya kampeni kuchagua kati ya David Musila wa Jubilee na Julius Malombe wa Wiper.

“Utakayemchagua awe Malombe au Musila, itakuwa wewe kuamua kwa sababu tunataka kupeleka Ngilu Nairobi,” Raila alisema.

Aliongeza kuwa utawala wake, iwapo atashinda kura ya Agosti, utahakikisha kaunti zimetengewa zaidi ya asilimia 35 ya sehemu ya mapato. Kuhusu chaguzi za chama, kiongozi huyo wa ODM alisema wakazi walikuwa huru kuchagua mgombeaji yeyote kutoka 26 wanaounda chama cha muungano cha Azimio la Umoja.

"Tuna Jubilee, ODM, Narc, Narc Kenya katika timu ya vyama 26... Ni nyinyi kuamua ni nani wa kumpigia kura miongoni mwa vyama kwani sote tuko Azimio," akasema.

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved